Mashindano ya baiskeli Vodacom Mwanza Open Cycle Challenge yarindima jijini Mwanza...ARUSHA YATISHAA

By Gadiola Emanuel - 1:14:00 PM

Hatimaye Richard Laizer wa mkoani wa Arusha ndiye ametegua kitendawili cha nani anayepaswa kuwa mshindi wa mbio za wazi za baiskeli za Vodacom Mwanza Open Cycle Challenge baada ya kuwashinda washiriki wengine zaidi ya 400 walijitokeza kushiriki kwenye mashindano hayo kwa upande wa wanaume.
 
Hapa mshindi huyo wa mbio za Mwanza Open Vodacom Cycle Challenge 2011 kutoka klabu ya Arusha Cycling Richard Laizer akipokea zawadi yake ya shilingi milioni 1.500.000 kutoka kwa Mkuu wa Udhamini wa Kampuni ya Vodacom Tanzania George Rwehumbiza mara baada ya kutajwa katika mbio hizo za kilomita 196 zilizoanzia Busanda mkoani Shinyanga na kumalizikia Bugando Hills jijini Mwanza.
Picha kulia ni Steven Kingu Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Kanda ya Ziwa na kulia kwa George Rwehumbiza ni Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti SBL. Mdhamini mkuu wa mashiundano hayo ni kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom ikishirikiana na wadhamini wenza kampuni ya bia ya Serengeti SBL na Kituo cha Radio cha Clouds Fm.
Richard Laizer wa mkoani wa Arusha ndiye akionyesha zawadi zake mara baada ya kukabidhiwa rasmi jioni ya leo kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Morris Njowoka Meneja wa kinywaji cha Malta Guinness akimkabidhi zawadi mmoja wa washindi wa wa mbio za baiskeli za Vodacom Mwanza Open Cycle Challenge.
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti SBL Ephraim Mafuru akikabidhi zawadi kwa Zavalina Abel aliyeshiriki katika mbio za kilomita 10.
Wadau wakipozi kwa picha kutoka kulia ni G. Sengo wa Clouds Mwana, Amicus Butunga wa TBC Mwanza, mkuu wa kambi John Bukuku (Mzee wa Full Shangwe blog)  na mwisho ni Moriss Njowoka Meneja wa kinywaji cha Malta Guiness. Hii ndiyo timu ya Arusha Cycling iliyofanya vizuri kwa uoanda wa wanawake na wanaume kama unavyowaona na wamependeza kweli kwa vivazi vyao.
Mkurugenzi wa masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti SBL Ephraim Mafuru akimpongeza Sophia Husein kutoka klabu ya Arusha Cycling aliyeshinda kilomita 80 wanawake baada ya kupokea zawadi zake kulia ni Moriss Njowoka Meneja wa kinywaji cha Malta Guiness..
Richard Laizer wa mkoani wa Arusha akipongezwa na mashabiki wake mara baada ya kumaliza mashindano hayo katika vilima vya Hospitali ya Bugando jijini Mwanza.
Mmoja wa washiri akimalizia mbio hizo.
Mkurugenzi wa masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti SBL Ephraim Mafuru akijadiliana jambo na Stanslaus Mbaga Mkuu wa Masoko Kanda ya Ziwa na Anold Kileo Meneja wa matangazo.
M ashabiki mbalimbali wakiwa katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakishuhudia utoajiwa zawadi kwa washindi.
Huyu baada ya Baiskeli yake kumzingua akaamua kumalizia mbio kwa kukokota huku akikimbia.
Huyu naye uvumilivu ulimshinda akaruka kwenye baiskeli mara tuu baada ya kuvuka mstali wa kumaliza mashindano.
Richard Lasizer akimalizia mbio katika kituo cha mwisho.

  • Share:

You Might Also Like

0 comments