AMBASSADORS OF CHRIST FROM KIGALI NDANI YA TAMASHA LA PASAKA

By Gadiola Emanuel - 9:04:00 AM

amNa Mwandishi Wetu
 IDADI ya wasanii wa nje watakaokuja kutumbuiza kwenye Tamasha la Pasaka mwaka huu imezidi kuongezeka na sasa Wanyarwanda nao wamethibitisha kushiriki. Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema jana kuwa kwaya ya Ambassadors of Christ ya Kigali Rwanda inayotamba na albamu ya Mtegemee Yesu imethibitisha kushiriki tamasha hilo litakalofanyika Machi 31 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
 
 “Watakuja kung’arisha tamasha la mwaka huu na wamejipanga vya kutosha kuhakikisha mashabiki wanapata burudani ya nguvu, nia yetu ni kuwa na wasanii wakubwa Afrika na hilo ndilo tutakalolifanya mwaka huu.
 “Kabla ya Jumatano tutatangaza msanii mkubwa mwingine ambaye bado tunaendelea na mazungumzo naye kuhakikisha mambo yanakuwa safi, ili aje kutumbuiza kwenye tamasha letu,” alisema Msama. Alieleza kuwa katika albamu yao hiyo ina nyimbo nane ambazo ni JY’ Ushima Uwite, Mtegee Yesu, Ndifuza Kugerayo, Iyana Iby’ Isi, Yesu Niwe Mungeri, Parapanda, Abasaruzi na Nenda.
 
 Wasanii wengine wa nje ya Tanzania ambao tayari wamethibitisha kushiriki tamasha hili ni , Ephraim Sekeleti wa Zambia na Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi Kenya. Wasanii wa Tanzania ni Rose Muhando, Upendo Nkone na John Lissu.
 Tamasha la Pasaka litafanyika Dar es Salaam Machi 31 na  litaendelea Aprili mosi kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, wakati Aprili 3 ni Uwanja wa Samora Iringa na Aprili 6 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na siku inayofuata itakuwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

  • Share:

You Might Also Like

0 comments