BAVICHA ARUSHA AANDIKA HAYA KUHUSU IGUNGA

By Gadiola Emanuel - 5:23:00 AM

 
Nachukua fursa hii,kuwashukuru WanaIgunga(Ingawa wengi hawana uwezo wa kuwa kwenye computer kama mimi na wewe)Nawashukuru wote waliotutia moyo,nawashukuru hata wale ambao hawakututia moyo,Nawashukuru sana
Uchaguzi Igunga umeisha,mengi yamesemwa na kuandikwa kuhusu mchakato mzima,kuna mengi sana yalitokea na mimi nimeyashuhudia.Kwanza nikiri kuwa ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika Igunga,kimsingi nilitarijia Igunga yenye neema,na maisha bora,lakini nilikumbana na UFUKARA wa kutisha,na maeneo mengine hata Kiswahili hawajui kwani vijana wadogo sana wa umri chini ya miaka 25 hawajaenda shule,amezaliwa hapo hapo kijijini,amekulia hapo kijijini,na hajui maisha mengine zaidi ya maisha ya shida hapo kijijini.Wanawake wanatembea hadi kilometa 15 kufuata maji ambayo kimsingi si safi wala salama.
Lakini katika lindi kubwa la umaskini wa Igunga,bado serikali ya CCM imatumia mabilioni ya pesa kurudisha jimbo la IGUNGA,ni wazi siasa za Igunga zilikuwa za nguvu kupita kiasi,kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifa letu tumeshuhudia uvunjivu,mkubwa wa sheria na katiba.Mimi ni mmojawapo wa waadhirika wakubwa wa siasa za visasi,na matumizi makubwa ya nguvu,nilitekwa na vijana wa green guard,na kunitupa porini,baada ya purukushani kubwa,nikaripoti polisi lakini hakuna hatua zilizochukuliwa,na mwisho wakanigeuzia kibao et mimi ndio niliwateka,(Aibu kwa jeshi letu la polisi,historia itawahukumu)
Nimeshuhudia dini ikiingilia siasa,na kuwataka waumini wao kutokichagua chama fulani,huu ni moto uliopandikizwa kwa makusudi kabisa,yaani chama tawala kimeishiwa hoja,hata kufikia mahali pa kuwatumia viongozi wa DINI,ili tu kujihakikishia uhalali wa kubaki madarakani,na bila aibu viongozi wetu wastaafu,na wazee wa heshima kwenye hili taifa wakakaa kimya,hakuna hata mmoja aliyekemea tabia hii(Historia itahihukumu ccm kwa kkupandikiza chuki ya dini kwenye taifa letu,aibu kubwa kwa ccm)
.Nimeshuhudia wanawake wakinyanyaswa na polisi eti tu ni wafuasi wa CHADEMA,hakuna hata mmoja aliyekemea,DC aliyevunja sheria yeye kwa kuwa tu ni DC na ni kada wa ccm,akaonekana amedhalilishwa.Nimeshuhudia vijana wengi wakibambikiziwa kesi,kwa kuwa tu ni wafuasi wa CHADEMA,ninapoandika sasa kuna vijana watano walishika gari ya mwenyekiti wa ccm wilaya ya Igunga akigawa hela rushwa,wakaripoti polisi,na baada ya polisi kukagua gari hiyo wakakuta begi lina zaidi ya 21milion,vijana wale wazalendo wakawekwa chini ya ulinzi,eti ni wanyanganyi wanotumia silaha,na bila utu wala heshima kwa binadamu wenzao,polisi wakawapelea Nzega siku ya Ijumaa,hadi Jumatatu walipopelekwa mahakamani na kusomewa shitaka la unyanganyi wa kutumia silaha,Vijana wale walisekwa ndani kwa siku tatu bila chakula wala maji,,u wapi utu wa na usawa wa binadamu?tunaelekea wapi kama taifa?na misingi gani ya taifa tunajenga?
Uchaguzi wa Igunga umekuwa na mengi ya kujifunza,kwa serikali ya ccm,wametumia rasilimali zetu,kwa ajili ya Igunga tu,ni aibu kwa ccm na viongozi wake,lakini kubwa na ambalo sharti wajifunze ni kuwa ,inapofika mahali Chama dola,chenye serikali,rasilimali pesa,rasilimali watu,uongozi kuanzia balozi wa nyumba kumi,kulalamikia CHAMA CHA UPINZANI,eti kinagawa hela,eti kimeingiza makomandoo,na Mungiki,ni wazi kuwa CCM kimepoteza mwelekeo na sasa kinaelekea kwenye anguko kuu.
Kimsingi Dr Kafumu hajachaguliwa na wanaIgunga,amewekwa na DOLA na DOLA hiyohiyo itamwondoa,ni swala la muda,kwa ukiukwaji huu wa sheria,kanuni,utu wa binadamu,kamwe hatodumu kwenye kiti cha DAMU,kwa zaidi ya mwaka.
Ni faraja iliyoje kuona kuwa sasa ukombozi wa pili wa taifa letu u karibu kuliko mategemeo ya wengi,kuna wengine wataona ni maneno ya kujifariji baada ya kushindwa Igunga.Lakini huu ndio ukweli na ccm ni mashahidi katika hili,wanajua nguvu kubwa kiasi gani walitumia kulikomboa na kutunyanganya ushindi Igunga,na bila msaada wa vyombo vya dola wasingeweza.
Uchaguzi umeisha,kuna majeruhi wengi,na ambao kesho ndio wapamabanaji wa ukweli,Jambo moja la msingi ni kwamba hakuna wingi wa silaha,risasi,mabomu,wala vifaa vya kisasa vya kijeshi vinavyoweza kuzuia umma unaotaka mabadiliko,umma uliochoka,umma unaolilia ukombozi,na kwa kadri serikali inavyozidi kuminya uhuru na demokrasia ndivyo umma unavyozidi kuamka na kupigania uhuru wao.Daima tutasonga mbele
Aluta continua…..
Na saa ya ukombozi ni sasa.............

Nanyaro
Ephata Nanyaro diwani kata ya Levolosi,Arusha-BAVICHA

  • Share:

You Might Also Like

0 comments